MKUU WA WILAYA YA ARUSHA AMEWEKA JIWE LA MSINGI KATIKA KITUO CHA AFYA

Mkuu wa wilaya ya Arusha Mjini Fabian Daqaro ameweka jiwe la msingi katika kituo cha afya kinachojengwa kata ya Mushono halmashauri ya jiji la Arusha ambapo kitakapokamilika kitahudumia wananchi zaidi 20,698 katika eneo hilo.
Akizungumza baaada mara baaada ya kuweka jiwe la msingi mkuu  wa Wilaya Fabian  Daqaro amesema serikali ya awamu ya tano chini ya Raisi Magufuli inahakikisha vituo vya  afya vinakuwa karibu na wananchi kupata uduma kirahisi ili kupunguza tatizo la wananchi  kufuata huduma umbali mrefu.
Akisoma taarifa kuhusu kituo hicho cha afya Mushono mganga mkuu wa jiji la Arusha Dokta Simon Chacha amesema kuwa kituo hicho kinajengwa kwa awamu mbili awamu ya kwanza ni kujenga msingi na ya pili ni kujenga boma pamoja na kupaua.
Kwa upande wa diwani wa kata na wananchi wa Mushono wamesema kuwa wanaishukuru serikali ya awamu ya tano kwa kuwasogezea wananchi huduma karibu zaidi na kituo hicho kitakapo kalimika kita wapunguzia adha ya kutembea kwenda mjini kiutafuta huduma ya Afya.
Mkurugenzi wa jiji la Arusha Adhuman Kihamia amesema malengo ya kituo hicho ni kuanza kufanya kazi rasmi mwezi wa sita lakini ifikapo mwezi wa tatu kitaanza kufanya kazi rasmi kikiwa na maitaji yote muhimu.

Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA