KESI INAYOWAKABILI BAADHI YA MAAFISA WA BENKI YA POSTA TABORA IMEENDELEA KUAHIRISHWA

Kesi Ya Uhujumu Uchumi Inayowakabili Baadhi Ya Maafisa Wa Benki Ya Posta Imeendelea Kuahirishwa Katika Mahakama Ya Hakim Mkazi Mkoa Wa Tabora Baada Ya Upande Wa Jamhuri Kushindwa Kuwasilisha Mahakamani Hapo Hatua Ya Maelezo Iliyofikiwa Ya Upelelezi Wa Shauri Hilo.
Mbele Ya Hakim Mkazi wa Mahakama Tabora EMANUEL NGIGWANA Wakili Wa Serikali TITO MWAKALINGA Ameieleza Mahakama Kuwa Anaendelea kufanya Mawasiliano na Mawakili Waliopo Kwenye Ofisi Ya Mkurugenzi Wa Makosa Ya Jinai Nchini DPP Kuhusu Hatua iliyofikiwa ya Upelelezi wa Jalada hilo.
Jopo La Mawakili Upande Wa Washitakiwa Wakiongozwa Na Wakili PAULUSI RWEYONGEZA Walitaka Kujua Mahakamani Hapo Kama Shauri Hilo Limetelekezwa Au La Kwa Kuwa Watuhumiwa Wanaendelea Kusota Mahabusu huku wakiwa Wametenganishwa na Familia zao ambazo bado zinaendelea kuwategemea.
Akijibu Hoja Hiyo Wakili Upande Wa Jamhuri TITO MWAKALINGA Ameomba Mawakili Waelewe Kuwa Shauri Hilo Bado Linafanyiwa Kazi Kisheria Na Kwamba Ofisi Ya DPP Haijawahi Kuichezea Mahakama kama walivyokuwa Wamedai.
Kwa Upande Wake Hakim Mfawidhi Wa Mahakama Hiyo EMANUEL NGINGWANA Amesema Kuwa Ofisi Ya DPP Itimize Majukum yake Kisheria ili Haki Iweze Kutendeka.
Kesi Ya Uhujumu Uchumi Namba Tatu Ya Mwaka 2017 Inayo Wakabili Watuhumiwa 16 Wakiwemo Baadhi ya Maafisa Wa Benki ya Posta Imeahirishwa Hadi Novemba 29 Mwaka Huu Itakapo Tajwa Tena.

Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA