RAIS AMEMTUMBUA MKURUGENZI MTENDAJI MWINGINE



Na.Issack Gerald
Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh.Dkt John Pombe Magufuli ametengua uteuzi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru Bw.Abdallah Hussein Mussa kwa kushindwa kumudu majukumu yake.
Katibu mkuu wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na serikali za mitaa TAMISEMI Mhandisi Mussa Iyombe ametoa taarifa hiyo ya kutenguliwa kwa mkurugenzi huyo leo mjini Dodoma.
Kwa mjibu wa Mkuu wa kitengo cha mawasiliano serikalini Rebecca Kwandu,uteuzi wa Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru utafanywa baadaye.
Wiki iliyopita Rais Magufuli alitengua nafasi ya wakurugenzi wa tendaji wawili wa Manispaa ya Bukoba na Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba.
Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA