CHANZO CHA BOMU KUUA WANAFUNZI 9 MKOANI KAGERA HIKI HAPA



Na.Issack Gerald
Kamanda wa jeshi la polisi Mkoani Kagera Agustino Olomi amesema chanzo cha wanafunzi kupoteza maisha na kujeruhiwa kwa bomu ni kutokana na Mwanafunzi kuokota bomu hilo akidhani chuma chakavu ili akauze.
Katika taarifa aliyoitoa akizungumza na Wanahabari Kamanda Olomi amesema,katika kijiji hicho kumekuwa na tabia ya kuuza vyuma chakavu ambapo mnunuzi huwa akiwapatia malipo ya madaftari.
Kwa upande wa Kamanda wa Kikosi cha kulinda mipaka cha Jeshi la Wananchi wa Tanzania JWTZ wilayani Ngara Meja TR Mutaguzwa amesema,Bomu hilo lilikuwa na vipande 36 na lingelipukia ndani ya darasa lingeleta athari zaidi .
Jumla ya wanafunzi 9 walifariki dunia na wengine 25 kujeruhiwa kutokana na mlipuko wa bomu hilo.
Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA