NDEGE YA MIZIGO IMEANGUKA IVORY COAST

Mabaki ya ndege hiyo aina ya Turboprop yalisombwa hadi katika ufukwe ambapo waokoaji walionekana wakiwatibu watu walionusurika.
Ndege moja ya mizigo nchini Ivory Coast imeanguka katika bahari muda mfupi baada ya kuondoka mji mkuu wa Abidjan huku watu watatu wakidaiwa kufariki na wengine wakijeruhiwa.

Mabaki ya ndege hiyo aina ya Turboprop yalisombwa hadi katika ufukwe ambapo waokoaji walionekana wakiwatibu watu walionusurika.
Kwa mjibu wa mtandao wa Koac ndege hiyo ilikuwa ikibeba mizigo ya jeshi la Ufaransa ambapo inasemekana imeanguka wakati wa mvua kubwa karibu na bandari ya Bouet.
Shahidi mmoja amesema watu wanne walifariki huku miili miwili ikitolewa kutoka katika ndege hiyo huku mingine miwili ikionekana katika mabaki ya ndege hiyo.
Vyombo vya habari na tovuti ya Ivoire Matin viliripoti vifo vya watu watatu huku watu sita wakijeruhiwa ambapo Mtu mmoja amekamatwa na Ndege hiyo imedaiwa kutengezwa nchini Ukrain.

Habari zaidi ni www.p5tanzania.blogspot.com au ukurasa P5Tanzania Limited

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA