RAIS MAGUFULI ATUMA SALAMA ZA RAMBIRAMBI WALIOFARIKI AJALI YA BASI LA CITY BOY,ATOA MAAGIZO
Rais John Magufuli ametuma salamu za
rambirambi kufuatia ajali ya basi la kampuni ya City Boy iliyotokea jana Aprili
4,2018.


Taarifa iliyotolewa leo Alhamisi
Aprili 5,2018 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu,Gerson Msigwa imesema
Rais Magufuli mbali na kutoa pole,amewataka
viongozi wote wanaohusika na usimamizi wa usalama barabarani kutafakari kwa nini
ajali nyingi zimekuwa zikitokea katika maeneo yaleyale na kutafuta ufumbuzi ili
kuepusha madhara ya watu kupoteza maisha,kupata ulemavu wa kudumu na kupoteza
mali.
Rais amemtaka Mkuu wa Mkoa wa Tabora,Aggrey
Mwanri kufikisha salamu zake za pole kwa
wafiwa wote na amewaombea marehemu wote
wapumzishwe mahala pema peponi huku akiwapombea majeruhi wapone haraka.
Habari zaidi ni www.p5tanzania.blogspot.com
Comments