JWTZ WAONYA WANAOJIHUSISHA NA UTAPELI WA AJIRA JESHINI


Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) limewaonya wote wanaojihusisha na utapeli wa ajira jeshini ambapo limesema litaendelea kuchukulia hatua kali zaidi.


Hayo yamesemwa leo na Msemaji Mkuu wa jeshi hilo,Kanali Ramadhan Dogoli wakati akizungumza na waandishi wa habari makao makuu Upanga-Dar es Salaam.
Amesema kuwa kuna baadhi ya majangili hujifanya kuwa ni watumishi wa jeshi hilo na kuwatapeli wananchi na hivyo wananchi wametakiwa kuwa makini.
Aidha Dogoli amesema askari ambao wamekuwa wakiwabaini wamekuwa wakiwapatia adhabu ndogo ya kuwafukuza kazi na wengine wanafikishwa mahakamani.
Kumekuwa kukiripotiwa matukio ya wananchi kutapeliwa na watu wanajifanya kuwa ni watumishi wa jeshi wakisema wanawatafutia nafasi za ajira jeshini ambapo mwishoni imekuwa tofauti.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA