MAJAMBAZI YAVAMIA NA KUPORA SADAKA KANISANI


Majambazi wamevamia Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Theresia wa Mtoto Yesu-Mbezi Mwisho jijini Dar es Salaam na kupora fedha na baadhi ya vifaa vya kuendeshea misa usiku wa kuamkia leo.

Mwenyekiti wa Kamati ya Mipango,Uchumi na Fedha wa parokia hiyo,Arnold Kimanganu amesema majambazi hao waliwapiga walinzi kabla ya kuingia kanisani.
Paroko wa parokia hiyo,Sunil Kishor amesema majambazi hao walivamia kanisa hilo saa tisa usiku na wameiba fedha na baadhi ya vifaa vya kuendesha misa.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam,Lazaro Mambosasa amekiri kutokea kwa tuki hilo japo amesema hajapata taarifa ya kimaandishi ofisini kwake.
Habari zaidi ni www.p5tanzania.blogspot.com

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA