MUIGIZAJI MAARUFU NCHINI INDIA,SALMAN KHAN AHUKUMIWA JELA MIAKA MITANO


Muigizaji mkongwe nchini India, Salman Khan amehukumiwa kwenda jela miaka mitano baada ya kukutwa na hatia ya kuua wanyama jamii ya swala miaka 20 iliyopita.
Leo Aprili 05,2018 Mahakama Kuu mjini Jodhpur katika jimbo la Rajasthan nchini India imetoa hukumu hiyo baada ya kumkuta na hatia, huku waigizaji wenzake Saif Ali Khan, Tabu, Sonali Bendre na Neelam Kothari wakiachiwa huru baada ya kukutwa hawana hatia.
Salman Khan (52) alishtakiwa kwa kosa la ujangili kwa kuua wanyama hao (BlackBuck Antelopes) ambao ni wachache nchini India mnamo mwaka 1998.
Kwa mujibu wa mtandao wa Daily Mail, Salman Khan alifanya tukio hilo katika kijiji cha Kankani wakati aki-shoot filamu yake ya Hum Saath Saath Hain akiwa na wasanii wenzake watano ambao wameachiwa leo.
Habari zaidi ni www.p5tanzania.blogspot.com  

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA