RAIS KUZINDUA UKUTA WA MIGODI YA TANZANITE


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.John Magufuli kesho Aprili 6,2018 anatarajia kuzindua ukuta wa machimbo ya madini wa Mirerani mkoani Manyara.
Hayo yamesemwa leo na Msemaji Mkuu wa jeshi hilo,Kanali Ramadhan Dogoli wakati akizungumza na waandishi wa habari makao makuu Upanga-Dar es Salaam.
Kanali Dogoli amesema shughuli itaanza saa moja na wananchi wanakaribishwa kushuhudia uzinduzi huo.
Mwishoni mwa mwezi Septemba mwaka 2017Rais wa Tanzania John Magufuli aliliagiza Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ) kujenga ukuta wa kuzunguka vitalu vya kuanzia A hadi D vyenye madini ya Tanzanite katika eneo la Mererani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara ili kudhibiti uchimbaji na biashara ya madini hayo.
Rais Magufuli alitoa agizo hilo kwenye sherehe ya ufunguzi wa barabara ya Kia - Mererani iliyofanyika katika eneo la Mererani.
 Habari zaidi ni www.p5tanzania.blogspot.com

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA