BASI NA FUSO ZAUA 12 NA KUJERUHI

Watu 12 wamefariki dunia na wengine 46 kujeruhiwa baada ya basi la abiria la City Boy kugongana uso kwa uso na fuso usiku wa kuamkia leo,Aprili 05, 2018 katika kijiji cha makomelo wilayani Igunga mkoani TABORA
Basi la City Boy lilikuwa likifanya safari yake kutoka Karagwe kwenda Dar es Salaam na imetokea baada ya kudaiwa dereva wa fuso kutaka kukwepa shimo na kujikuta fuso hilo likimshinda hivyo  kupelekea kugongana uso kwa uso
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tabora,Wilbrod Mutafungwa amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na tayari majeruhi wamepelekwa hospitali.
Hata hivyo,jeshi la polisi limeahidi kutoa taarifa zaidi leo baadaye ikiwemo na hali ya majeruhi wa ajali hiyo.
Habari zaidi ni www.p5tanzania.blogspot.com

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA