HALMASHAURI YATOA TAHADHARI KWA WAZAZI KUPELEKA WATOTO KATIKA SHULE ZISIZOSAJILIWA


Na.Issack Gerald
Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi imetoa tahadhari kwa wazazi Mkoani Katavi wanaowapeleka watoto wao katika shule mbalimbali za Manispaa ambazo hazijasajiliwa.
Kauli hiyo imetolewa na Afisa elimu taaluma Manispaa ya Mpanda Mwalimu Rashid Pili wakati akizungumza kuhusu uwepo wa baadhi ya shule ambazo hazijasajiliwa lakini tayari zikiwa zimesajili wanafunzi wa shule za msingi na chekechea.
Kwa mjibu wa Mwalimu Pili,Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda ina Shule 36 zikiwemo 34 za serikali na 2 za binafsi za Reimeta na Nzela English Pre-Primary School zinazotambuliwa na serikali ambapo mtoto anayesajiliwa nje ya shule hizo hatambuliki katika mfumo wa elimu Tanzania.
Hata hivyo Mwalimu Pili amesema Ijumaa ya Wiki hii wanatarajia kukutana na wamiliki wa shule hizo ili kufikia mwafaka ili kuendesha mambo kwa kufuata misingi ya sheria na kanuni za nchi.
Aidha Mwalimu Pili amesema katika mwaka 2018 manispaa ya Mpanda imejipanga kufaulisha kwa karibu asilimia 99 ili kurejea katika nafasi ya kwanza iliyokuwa nayo katika kipindi cha mwaka 2016,2015 na 2014.
Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA