DIWANI ATAKA MKURUGENZI ATAFUTE MAENEO KWA AJILI YA WAPIGA KURA WAKE


Diwani wa Kata ya Mpanda Hotel Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi Mh.Willium Liwali amemshauri Mkurugenzi mtendaji Manispaa ya Mpanda kutafuta mahali pa kuwaweka wafanyabiashara wadodo wadogo wapatao 200 wa kata hiyo waliokosa nafasi ya kufanyia biashara.
Mh.Liwali amesema hayo kufuatia agizo la Mkurugenzi wa Manispaa ya Mpanda Michael Nzyungu kuagiza wafanyabiashara wote walio katika masoko yasiyo rasmi katika Manispaa hiyo kutakiwa kuondoka na kufanyia biashara zao katika masoko rasmi.
Kwa mjibu wa Diwani Liwali masoko yote ambayo wafanyabiashara hao wangehamia yakiwemo soko la Mpanda Hotel lililopo kata ya Majengo na soko la Kachoma lililopo kata ya Makanyagio yote yamejaa.
Wiki iliyopita,mamia ya wafanyabiashara wadogowadogo wanaofanyia biashara zao katika machinjio ya ng’ombe Mpanda Hotel waliandamana mpaka kituo cha Radio Mpanda Fm wakipinga agizo la Mkurugenzi anayewataka kuondoka katika maeneo hayo yasiyo rasmi.
Kwa mjibu wa agizo la Mkurugenzi Michael Nzyungu,wafanyabiashara wote walio katika maeneo yasiyo halali kwa biashara walitakiwa wawe wameondoka mpaka kufikia Januari 22 mwaka huu suala ambalo mpaka sasa limeshindikana.
Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA