TIMU YA CCBRT SASA NI MKOANI KIGOMA

 Kampeni ya uhamasishaji wa matibabu ya ugonjwa wa  fistula inayoendeshwa na CCBRT inayofanyika Tanzania nzima,hivi sasa timu ya uhamasishaji matibabu ya ugonjwa huo mkoani Kigoma.
Akiongea na timu hiyo mkuu wa mkoa wa Kigoma Bregedia mstaafu Emanueli Maganga ameeleza kufurahishwa kwake na juhudi zinazofanywa na CCBRT na kubariki ujio wa timu hiyo kwani utasaidia katika kueneza elimu juu ya ugonjwa huo kwa wakazi wa kigoma.
Kwa upande wake meneja wa mradi wa fistula kutoka hospitali ya CCBRT iliyoko Msasani jijini Dar es salaam Bwana Clement Ndahana amesema kuwa kwa kila mwaka zaidi ya akina mama 3000 nchini hupata ugonjwa wa fistula lakini akina mama 1400 ndio ambao hupata matibabu ya ugonjwa huo.
Mara baada ya salamu mkoani humo timu hiyo ya uhamasishaji imeelekea wilayani uvinza kijiji cha Kalia kilichopo mwambao wa ziwa Tanganyika ambako wataanza  na uhamasishaji wa matibabu ya ugonjwa wa fistula mkoni humo.
Chanzo:Isaac Isaac,Mhariri-Issack Gerald

Habari zaidi ni www.p5tanzania.blogspot.com au ukurasa P5Tanzania Limited

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA