WANANCHI MKOANI TABORA WAMETAKA KITUO CHA POLISI KIFUNGULIWE



Wananchi wa kata ya Loya wilaya ya uyui mkoani tabora wameomba kufunguliwa kituo cha polisi katani humo kwa lengo la kukabiliana na matukio ya uharifu.
Kata hiyo pamoja na kata nyingine nne hazina kituo cha polisi hali inayowalaizimu kutembea umbali wa zaidi ya kilometa 150 kufuata huduma za kipolisi katika kata ya Kigwa.
Wakizungumza katika mkutano wa hadhara mbele ya kamanda wa polisi mkoa wa tabora ACP Wilbrod Mutafungwa wananchi hao wamesem kwa sasa wanakabiliwa na matukio mbalimbali ya uharifu ikiwemo wizi lakini imekuwa vigumu kudhibiti uharifu katika maeneo hayo kwa kuwa hakuna kituo cha polisi.
Kamanda Mutafungwa baada ya kukagua jengo la kituo cha polisi katani hapo,ametoa muda wa wiki mbili kwa viongozi wa kata na wilaya kukamilisha ukarabati wa jengo la kituo cha polisi ili kifunguliwe na kuanza kuwahudumia wananchi.
Wananchi wa kata ya Loya na kata jirani wanaamini kufunguliwa kwa Kituo hicho cha polisi kitakuwa mkombozi wa matukio mbalimbali ya uharifu.
Habari zaidi ni www.p5tanzania.blogspot.com au ukurasa P5Tanzania Limited

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA