MWAFAKA WA UGAWAJI VIWANJA KUPATIKANA LEO MKOANI KATAVI



Na.Issack Gerald-Katavi
SERIKALI za mitaa ya Msasani na Tambukareli Manispaa ya Mpanda,leo zinatarajia kufanya mkutano wa hadhara kwa ajili ya kupata mwafaka wa namna ya kugawa viwanja kwa wahanga wa bomoa bomoa.

Mwenyekiti wa mtaa wa Msasani Bw.Jonard Makoli amesema mkutano huo unatarajiwa kufanyika kuanzia majira ya saa 8 mchana.
Mkutano huo unafanyika ikiwa tayari kuna malalamiko kutoka kwa wakazi wa mitaa ya Msasani na Tambukareli wakilalamika kutoridhishwa na mfumo wa ugawaji viwanja ambapo imeelezwa kuwa watakaopewa kipaumbele ni watu wasiokuwa na uwezo kama wazee na wagonjwa huku wananchi wengine wakisema ni mpango unaowaacha bila kujua hatima yao.
Viwanja 150 vilivyopo mtaa wa Kampuni kata ya Misunkumilo  vilinunuliwa na Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini Mh.Sebastian Kapufi ili vigawiwe bure kwa wakazi hao ambapo kwa mjibu wa Mstahiki meya wa Manispaa ya Mpanda Willium Mbogo kila mtaa utapata viwanja 75 kwa ajili ya wakazi wake.
Zaidi ya Kaya zipatazo 200 zinatarajiwa kubomolewa makazi yao ili kupisha bomoabomoa ili eneo la hifadhi ya reli ibaki wazi na wakazi hao wanatakiwa wawe wameondoka kabla ya mwezi Januari mwakani.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA