WAKULIMA WA KAHAWA KUTOKA KIGOMA KWENDA IKULU YA RAIS KUFIKISHA KILIO CHA MADAI YAO

Chama cha ushirika cha wakulima wa kahawa  (AMKOS) wilayani Buhigwe mkoani Kigoma,kimechagua wawakilishi watatu,kwa ajili ya kuwawakilisha wakulima hao kwa rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dr.John Pombe Magufuli.
Wawakilishi hao watamfikishia Mh.Rais madai yao wanayodai kwa viongozi waliopita  wa chama hicho,ambapo ni muda wa miaka miwili sasa.
Wamefikia maamzi hayo katika mkutano wa wanachama uliofanyika wilayani humo,kwa lengo la kujadili kuhusu madai yao wanayodai kwa viongozi waliopita wa chama hicho.
Mwenyekiti wa chama hicho,Bw.Issa Madamu amesema, wakulima hao wanadai jumla ya sh.mil.27 kwa viongozi hao waliopita tangu 2015.
Bw.Madamu amesema juhudi za kudai pesa hiyo,zimeenda hadi ngazi ya mkoa lakini bado hawajapata mafanikio na kwamba ndio maana wamechukua maamzi hayo ya kwenda kwa Rais ili wapatiwe ufumbuzi wa madai yao.
Aidha wakulima hao wameiomba serikali ya mkoa wa Kigoma kuwahimiza viongozi wa ngazi za chini kushughulikia matatizo ya wananchi wa hali ya chini ili kukuza na kuleta maendeleo kama Mh.Rais Magufuli anavyoagiza.
Habari zaidi ni www.p5tanzania.blogspot.com au ukurasa P5Tanzania Limited


Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA