WAKAZI WILAYANI MPANDA SERIKALI IWAJIBIKE KUTENGA MAENEO YA WAFUGAJI NA WAKULIMA

Baadhi ya wakazi wa kata ya Magamba Manispa ya Mpanda mkoani Katavi wameitaka serikali kutenga maeneo ya wafugaji na wakulima ili kuepusha migogoro ya ardhi inayojitokeza mara kwa mara
Wakizungumza kwa nyakati tofauti wananchi hao wamesema wakulima na wafugaji wanapoendesha shughuli zao katika eneo moja huchangia mifarakano isiyo ya lazima na kushauri wafugaji kutengewa eneo tofauti na wakulima ili kuondoa mwingiliano
Kwa upande wake Bi.Anna Thomas ambaye ni mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Magamba amekiri kuwepo kwa migogoro ya mara kwa mara baina ya wakulima na wafugaji na kuongeza kuwa inachangangiwa na wafugaji kuwa na mifugo mengi kwenye eneo dogo
Philemone Tesha Afisa kilimo wa kata ya magamba amesema serikali ina mpango wa kutenga maeneo ya kuchungia yatakayokuwa tofauti na mashamba japo hakubainisha wazi mpango huo ni lini utaanza kutekelezwa.

Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA