DKT.SHEIN ATOA MSAMAHA KWA WANAFUNZI 12 WANAOTUMIKIA CHUO CHA MAFUNZO ZANZIBAR

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein ametoa msamaha kwa wanafunzi 12 waliokuwa wakiendelea kutumikia vyuo vya Mafunzo vya Unguja na Pemba ikiwa ni miongoni mwa Sherehe za miaka 54 ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Dk.Abdulhamid Yahaya Mzee amsema Rais amechukua hatua hiyo kwa uwezo aliopewa chini ya kifungu cha 59 cha Katiba ya Zanzibar 1984.
Mh.Rais ameamuru kuwa kifungo kilichobaki cha wanafunzi walionufaika na msamaha huo ambao bado wanaendelea kutumikia katika vyuo vya Mafunzo vya Unguja na Pemba kuwa kipindi hicho chote kinafutwa na kwamba wanafunzi hao waachiwe huru kuanzia siku ya jana.
Taarifa hiyo imeeleza kuwa Zanzibar inasherehekea miaka 54 ya Mapinduzi ya Zanzibar 12 Januari 2018 na kwa kuwa Mhe.Rais ameridhika kuwa kuna sababu za kutosha za kutumia uwezo wake huo katika sherehe hii wanafunzi hao waachiwe huru.
Walionufaika na msamaha huo kwa Unguja ni Abdul-Azizi Abdalla Mohamed,Omar Abdalla Nuhu,Ali Khamis Mrau, Mussa Ali Vuai,Hassan Seif Khamis,Nassor Abeid Issa,Jihadi Jalala Jihadi na Edward Jeremia Magaja.
Aidha,wengine walionufaika na msamaha huo kwa upande wa Pemba ni Sleiman Abdalla Amir,Mtumwa Khamis Kaimu,Said Seif Omar na Masoud Seif Nassor.

Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA