NAIBU WAZIRI ATAKA WATOTO HAPA NCHINI WALINDWE NA KUPATIWA HAKI ZAO MANISPAA YA MPANDA NAO WAJA NA MKAKATI

Na.Issack Gerald
Naibu waziri wa Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dk.Faustine Ndugulile amewataka watanzania kuhakikisha watoto wote wanapatiwa haki zote za msingi katika maisha yao ikiwemo haki za kuishi na kulindwa.
Naibu waziri wa Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dk.Faustine Ndugulile
Dkt.Ndugulile ametoa wito huo jana Mjini Mpanda wakati akizungumza na Makundi mbalimbali ya wananchi ambayo yamepewa jukumu la kuelimisha jamii kuhusu haki za mtoto na kuwaibua watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi.
Aidha DK.Ndugulile amesema serikali itaendelea kushirikiana na Shirika la JSI la Marekani linalojihusisha na masuala ya jamii ikiwemo kudhibiti mambo yanayomkatisha mtoto kutimiza ndoto zake hasa kielimu.
Kwa upande wake Afisa Ustawi wa Jamii Manispaa ya Mpanda Bi.Redgunda Mayorwa amesema ushirikiano kati ya serikali na wadau mbalimbali ndiyo njia pekee itakayomukoa mtoto dhidi ya mazngira hatarishi ikiwa ni pamoja na wanaishi na maambukizi ya virusi vya Ukimwi.
Flora Cosmas kutoka Manispaa ya Mpanda ambaye ni Miongoni mwa watoa huduma ngazi ya jamii katika masuala ya mbalimbali ikiwemo ukatiri wa kijinsia pamoja na mambo mengine amesema Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda ina jumla ya wasimamizi wa mashauri ya watoto ngazi ya jamii wapatao 90 wakiwemo wanaume 40 na wanawake 50 huku wasimamizi viongozi wakiwa 15 wanaume 8 na wanawake 7.
Aidha amesema jumla ya watoto 1200 na wazazi walezi 506 waishio katika mazingira wameibuliwa na kupatiwa huduma katika maeneo mablimbali ya Manispaa ya Mpanda.
Katika Mkoa wa Katavi kumekuwa kukiripotiwa kesi kadhaa za watoto kunyanyaswa,kutupwa katika mazingira hatarishi mara baada ya kuzaliwa  na kutopatiwa haki za msingi ikiwemo elimu ambao nguvu ya jamii inatakiwa kutumika ipasavyo ili kukomesha matukio hayo ili kumlinda mtoto.
Ziara ya siku mbili ya Naibu waziri wa Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dk.Faustine Ndugulile ilihitmishwa jana mkoani Katavi.

Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA