SERIKALI KUSAMBAZA MAJI MAENEO MBALIMBALI MKOANI KATAVI KUTOKEA ZIWA TANGANYIKA



Na.Issack Gerald
Serikali imesema kuanzia mwaka wa fedha 2018/2019 wanatarajia kuweka fedha katika mradi wa maji Ziwani Tanganyika,ili kuwezesha kuvuta maji kutoka Ziwa Tanganyika na kusambazwa katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Katavi.
Kauli hiyo imetolewa leo bungeni Dodoma na Waziri wa maji na umwagiliaji Issack Kamwelwe,wakati akijibu swali la mbunge wa Mpanda vijijini Suleimani Kakoso aliyetaka kujua mpango wa serikali kuvuta maji kutoka Ziwa Tanganyika hadi Mpanda Mjini.
Waziri Kamwelwe ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Katavi Mkoani Katavi,amesema wizara imepokea andiko la mradi huo wa kuvuta maji kutoka ziwa Tanganyika na mradi huo utatekelezwa kama sehemu ya kumaliza tatizo la maji Mkoani Katavi.
Kwa sasa wakazi wa Mpanda wanapata maji kutoka vyanzo kama bwawa la milala na maji ya mseleleko Ikorongo.
Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA