FUSO YAUA 15 YAJERUHI 19 MKOANI RUKWA-Oktoba 5,2017

Na.Issack Gerald-Sumbawanga
Watu 15 wamefariki dunia na wengine 19 kujeruhiwa kufuatia ajali ya gari la mizigo aina ya Fuso.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa Geoge Kyando amethibitisha tukio hilo na kusema Lori hilo aina ya Fuso likiwa limebeba shehena ya viroba vya mahindi na watu 28 ndani yake limepinduka baada ya dereva kukata kona akiwa kwenye mwendokasi na kupelekea vifo hivyo.
Amesema gari hilo lilikuwa likitoka Sumbawanga kuelekea Wampembe katika mwambao wa ziwa Tanganyika wilayani Nkasi mkoani Rukwa usiku wa kuamkia jana.
Aidha Kamanda amesema Mbali na barabara kuwa ya milima na mteremko mkali kutajwa kuwa mojawapo ya chanzo cha ajali pia inasemekana dereva aliugua ghafla gari likiwa katika mwendo.
Hata hivyo dereva aliyekuwa anaendesha baada ya Yule wa awali kuugua,ametoweka kwa kukimbilia kusikojulikana baada ya ajali ambapo mmliki wa gari anasakwa na polisi ili sheria ichukue mkondo wake kufuatia gari hilo kubeba abiria kinyume na utaratibu wa magari yanayotakiwa.
Maiti 14 zimetambuliwa isipokuwa mtu mmoja aliyejulikana kwa jina Abubakari Amani(Madevu) hajatambulika ambapo maiti zote zimehifadhiwa katika hospitali ya mkoa waRukwa.
Mwezi uliopita watu watatu walifariki dunia na wengine watatu walijehiwa kufuatia ajali ya kupinduka kwa lori na mtu kugongwa huku ajali nyingine ya boti iliyosababisha vifo vya watu ikitokea ziwa Tanganyika.

Habari zaidi ni www.p5tanzania.blogspot.com au ukurasa P5Tanzania Limited

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA