TANZANIA YASHTUSHWA KUHUSISHWA NA KOREA KASKAZINI-Septemba 16,2017

Tanzania imesema imeshtushwa baada ya kuorodheshwa miongoni mwa nchi ambazo zimechunguzwa na Umoja wa Mataifa na kuhusishwa kuwa na uhusiano wa kibiashara na Korea Kaskazini.

Akizungumza katika mkutano wa waandishi wa habari jijini Dar es Salaam,waziri wa mambo ya nje Dkt.Augustine Mahiga,amesema licha ya uhusiano uliokuwepo awali, lakini tangu mwaka 2014,Tanzania imepunguza kabisa uhusiano wa kibiashara na kidiplomasia na nchi hiyo.
Aidha Waziri Mahiga amesema uhusiano huo wa kibiashara ulikuwepo kabla ya vikwazo vilivyowekwa hivi karibuni na Baraza la Umoja wa Mataifa.
Waziri huyo amesema anaelekea katika mkutano wa kawaida wa Umoja wa Mataifa, ambapo atatumia fursa hiyo kujibu tuhuma hizo kwa Baraza la Usalama.
Tanzania na Uganda ni miongoni mwa baadhi ya nchi zinazochunguzwa na Umoja wa Matiafa kwa tuhuma za kwenda kinyume na vikwazo vilivyowekwa na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa dhidi ya Korea Kaskazini.
Ripoti ya uchunguzi huo ilitolewa mnamo tarehe 9 mwezi wa Septemba. Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limesema linachunguza tuhuma za Tanzania kuingia mikataba ya kijeshi na Korea Kaskazini inayogharimu dola za kimarekani milioni 12.5.

Habari zaidi ni www.p5tanzania.blogspot.com

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA