WATATU KATA YA MPANDA NDOGO WAFIKISHWA MAHAKAMANI MPANDA WAKITUHUMIWA KUJIPATIA SHILINGI MIL.3,400,000/= KWA NJIA YA UDANGANYIFU


Na.Issack Gerald-Mpanda
WATU wawili wakazi wa kata ya Mpanda ndogo wilayani Mpanda mkoani Katavi, jana wamefikishwa katika mahakama ya mwanzo mjini Mpanda wakikabiliwa na shtaka la kujipatia fedha shilingi milioni tatu na laki nne kwa njia ya udanganyifu.

Mlalamikaji Bw. Lyango Joseph Mkazi wa Katumba ameiambia mahakama hiyo kuwa washtakiwa Mustafa Mfaume na Mohamed Salum walitenda kosa hilo la kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu kati ya mwaka 2014 na 2015.
Mbele ya hakimu wa mahakama hiyo Bw. David Mbembela, mlalamikaji Bw. Lyango Joseph amesema kuwa, mshtakiwa namba moja ambaye ni Bw. Mustaph Mfaume mnamo tarehe 20 mwezi desemba mwaka 2014 alienda nyumbani kwa Lyango Joseph na kuomba shilingi laki nne kwa lengo la lengo la kufanyia shughuli za kilimo cha tumbaku katika maeneo ya Kapemba kwa ahadi kuwa akiuza tumbaku atarudisha fedha alizokopa bila riba.
Mlalamikaji Bw. Lyango Joseph ameiambia mahakama hiyo kuwa mnamo tarehe 16 mwezi januari mwaka 2015 mshtakiwa namba moja aliongeza tena ombi la kukopeshwa shilingi laki nne kwa lengo lile lile. Amesema mnamo tarehe 05 mwezi februari mwaka 2015 aliomba akopeshwe tena shilingi laki tatu kwa ahadi ya kurejesha atakapouza tumbaku.
Mlalamikaji ameendelea kuiiambia mahakama ya mwanzo mjini Mpanda kuwa, mnamo tarehe 23 mwezi April mwaka 2015 mshtakiwa Mustafa Mfaume, aliomba tna akopeshwe shilingi laki sita lwa lengo lile lile la kuendeleza kilimo cha zao la tumbaku.
Bw. Lyango amesema mwezi April mwishoni tarehe ambayo mlalamikaji haikumbuki, mshtakiwa namba moja Bw. Mustafa Mfaume alikwenda tena nyumbani kwa mlalamikaji Kanoge ambaye ni rafiki yake wa muda mrefu na kuomba tena shilingi laki mbili ili aendeshee kilimo cha tumbaku na alikopeshwa fedha hizo na mwishoni mwa mwezi Mei tarehe ambayo mlalamikaji haikumbuki mshtakiwa namba moja Bw. Mustafa Mfaume alimpeleka mshtakiwa namba mbili Bw. Mohamed Salum  na kuomba amdhamini apewe shilingi laki mbili lakini mlalamikaji Bw. Lyango Joseph alikataa kwa kuwa hamfahamu na ndipo Mshtakiwa Mustafa Mfaume akadai anamdhamini, na kutokana na ukaribu na urafiki wao alikubali na kumkopesha kiasi hicho cha fedha.
Mlalamikaji amesema kwa mara ya mwisho mshtakiwa Mustafa Mfaume alikwenda kwake tarehe 12 mwezi Mei na aliomba fedha shilingi milioni moja na laki mbili ili zitumike kwenye shamba lake la tumbaku na kuahidi atakapouza na kupata malipo atarejesha fedha hizo bila riba.
Mlalamikaji Bw. Lyango Joseph amesema mshtakiwa namba moja Bw. Mustafa mfaume alikuwa amejipatia jumla ya shilingi milioni tatu na laki mbili na mshtakiwa namba mbili Bw. Mohamed Salum alijipatia shilingi laki mbili na kufanya jumla kuu ya fedha walizojipatia kwa udanganyifu kuwa shilingi milioni tatu na laki nne.
Awali washtakiwa wote wawili walitiwa hatiani na mahakama hiyo na kuhukumiwa kifungo cha miezi sita jela kutokana na kukiri kosa la kujipatia pesa kwa njia ya udanganyifu toka kwa Bw. Lyango Joseph na hukumu hiyo iliwataka watakapomaliza kutumikia adhabu ya kifungo jela, warejeshe fedha kwa mlalamikaji lakini baada ya kutoka jela hawakutekeleza amri ya  mahakama ya kumlipa mlalamikaji.
Mlalamikaji katika shauri hilo Bw. Lyango Joseph ametoa pia vielelezo vya hati 6 walizoandikiana pamoja na nakala ya uamuzi wa mahakama uliowatia hatiani washtakiwa. Washtakiwa wamekubali vielelezo vyote vilivyotolewa mbele ya mahakama ya mwanzo mjini Mpanda.
Hakimu wa mahakama hiyo Bw. David Mbembela amesema kwa kuwa washtakiwa hawajapinga nakala ya uamuzi wa mahakama iliyowatia hatiani, hata hivyo hati 6 zilizotolewa mahakamani kama kielelezo mahakama imezikataa mpaka zithibitishwe na kamishna wa viapo ili ziweze kutambulika kisheria kuwa ni hati halali.
Kesi hiyo imeahirishwa hadi tarehe 03 mwezi Februari mwaka huu, kungoja ushahidi kutoka kwa washauri wa mahakama waliosikiliza kesi hiyo tangu mwanzo ambapo hata hivyo hamimu Mbembela amesema dhamana kwa washtakiwa zinaendelea.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA