AFIKISHWA MAHAKAMANI MPANDA KWA TUHUMA ZA KUDHURU MWILI


Na.Boniface Mpagape-Mpanda
MTU mmoja mmoja mkazi wa Kasokola wilayani Mpanda Bw. Godfrey Kipyela, jana amefikishwa katika mahakama ya Mwanzo mjini Mpanda akikabiliwa na shtaka la kudhuru mwili.

Akisoma shtaka hilo, KIoplo Mtei wa jeshi la polisi Mpanda amesema mshtakiwa alitenda kosa hilo tarehe 13 desemba mwaka 2015, saa moja usiku maeneo ya Kasokola ambapo alimshambulia Bi. Maria January kwa kumpiga ngumi maeneo mbali mbali ya mwili na kumsababishia maumivu makali.
Hakimu wa mahakama ya Mwanzo mjini Mpanda Bw. David Mbembela baada ya kusikiliza maelezo ya mlalamikaji pamoja na ushahidi uliotolewa na mtoto mdogo mwenye umria wa miaka sita, amesema mlalamikaji anapaswa kuwasilisha mahakamani hati ya matibabu yenye muhuri kutoka hospitali alikopatiwa matibabu.
Kesi hiyo itasikilizwa tarehe 21 mwezi huu, na dhamana dhidi ya mshtakiwa inaendelea.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA