KATAVI YAPOKEA ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 80 ZA KUGHARIMIA ELIMU BURE.


Na.Issack Gerald-Katavi
Mkoa wa Katavi umepokea Zaidi ya Shilingi Milioni 80 kwa ajili ya kugharimia mpango wa serikali wa elimu bure kwa wanafunzi kuanzia Chekechea hadi  kidato cha nne.

Kaimu Afisa elimu Sekondari  Mwalimu Said Mwapongo amesema kuwa Mkoa wa Katavi umepokea zaidi ya milioni 80 na tayari zimesambazwa katika shule kwa ajili ya matumizi yaliyokusudiwa.
Afisa elimu Mwapongo,pamoja na kutoa wito kwa jamii,anatolea ufafanuzi wa michango hiyo ambayo imefutwa pamoja na ile inayopaswa kuchangwa.
Kuhusu wanafunzi waishio shule za bweni ambazo ni za Kata,Mwapongo amesema kuwa ziko kwenye mpango wa serikali wa kuziondolea michango inayotoka kwa wazazi kutokana na mpango wa wanafunzi waishio bweni kuwa katika mipango ya wazazi,walimu na bodi za shule.
Ufafanuzi huo wa Kaimu Afisa Elimu umekuja kufuatia malalamiko ya baadhi ya wazazi wakihoji kulikoni wanafunzi waendelee kuchangishwa michango ya vitu mbalimbali kama vyakula,pesa ya mlinzi na mpishi.
Mmoja wa wakazi kutoka kijiji cha Kabulonge Kata ya Litapunga Wilayani Nsimbo ambaye hakutaka jina lake litajweanasema yeye amekuwa na maswali mengi baada ya mtoto wake aliyeko katika Shule ya sekondari machimboni kuanmbiwa atoe michango wakati mtoto wake akipelekwa kuanza kidato cha kwanza.
Hata hivyo baadhi ya wazazi,walezi na jamii kwa ujumla imeonekana kutoelewa vizuri mchanganuo wa michango iliyofutwa na ilea ambayo jamii inapaswa kuendelea kuchagia.
Kwa Upande wake Afsisa elimu Sekondari Manispaa ya Mpanda Bi.Enelia Lutungulu amesema kuwa kesho wanatarajia kukutana na bodi za elimu kwa shule zilizo katika kata za Magamba,Kasokola na Shanwe kwa ajili kuweka sawa mazingira ya utekelezaji wa sera ya elimu bure.
Katika fedha hiyo Wilaya ya Mlele imepata zaidi ya Shilingi Milioni 32 kwa ajili ya elimu za msingi na  sekondari na huku hesabu ya kujua kiasi kilichopokewa kwa upande wa Wilaya ya Mpanda na Nsimbo kikiendelea kuchanganuliwa vizuri.
Idara ya elimu sekondari Mkoa wa Katavi kwa Ujumla imesema kuwa,wanaendelea kuweka mikakati ili kuhakikisha wanashika nafasi ya juu katika mithani ya taifa kwa ngazi ya shule za sekondari kama ilivyo kwa shule za Msingi ambapo Mkoa wa Katavi umeshika nafasi ya kwanza kwa mwaka 2015 huku Manispaa ya Mpanda ikishika nafasi ya kwanza kitaifa kwa miaka 2 mfululizo yaani mwaka 2014 na 2015.
Kwa mjibu wa barua ya tarehe 23 Novemba mwaka 2015 iliyoandikwa na Wizara ya Elimu na mafunzo ya ufundi na kusambazwa katika shule zote hususani za Sekondari Tanzania bara,inamtaka kila Mkuu wa shule kumpatia mwanafunzi fomu iliyotolewa na Wizara na siyo ile iliyokuwa ikiandaliwa na bodi au kamati za shule na lengo kuu likiwa kuondoa migogoro ya michango ya shule moja kutofautiana na shule nyingine Wakati huo huo barua ya Novemba 27 mwaka 2015 ikiainisha wajibu wa mzazi,mlezi,mwalimu,bodi au kamati za shule na jamii kwa ujumla.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA