WATATU WAFIKISHWA MAHAKAMANI KWA TUHUMA ZA MAKOSA MBALIMBALI LIKIWEMO SHAMBULIO LA MWILI.


Na.Issack Gerald-MPANDA
VIJANA watatu wakazi wa Mpanda mjini jana wamefikishwa katika mahakama ya Mwanzo mjini Mpanda, wakikabiliwa na shtaka la shambulio la kudhuru mwili.

Akisoma shtaka hilo Mbele ya hakimu David Mbembela, koplo Mtei kutoka jeshi la polisi Mpanda amewataja waliotenda kosa hilo kuwa ni Ramadhan Hamis mkazi wa Nsemulwa, Maneno Shaban mkazi wa Mikocheni na Mohamed Mussa ambapo wote kwa pamoja mnamo tarehe 14 Mwezi huu katika maeneo ya majengo mjini Mpanda, walimshambulia Abdallah Salum mkazi wa Misunkumilo na kumsababishia maumivu makali.
Koplo Mtei ameiambia mahakama kuwa mlalamikaji hakufika mahakamani kutokana na kulazwa katika hospitali ya wilaya ya Mpanda anakoendelea na matibabu kutokana na kipigo alichopigwa na washtakiwa hao.
Aidha, ameiomba mahakama hiyo isiruhusu dhamana kwa washtakiwa hadi pale taarifa kuhusu hali ya muhanga zitakapotolewa.
Washtakiwa wote wamekana shtaka na hakimu Mbembela amesema kutokana na ombi kutoka kwa askari ambaye ni afisa wa serikali na amekula kiapo cha kusema ukweli, hivyo mahakama imeridhia hoja iliyotolewa.
Kesi hiyo itatajwa tena tarehe 22 mwezi huu na washtakiwa wamerudishwa rumande.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA