WAKURUGENZI WAWILI WATUMBULIWA MAJIPU YUMO WA SULEIMANI LUKANGA WA MANISPAA YA MPANDA


Na.Mwandishi wetu-DAR ES SALAAM
MKURUGENZI Mtendaji Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi Suleiman Lukanga,amesimamishwa kazi kwa tuhuma za kuridhia na kutekeleza uamuzi ulioisababishia serikali hasara na upotevu wa fedha.
                                                       
Waziri George Simbachawene

Taarifa ya kusimamishwa kazi sambamba na Mkurugenzi Mtendaji Manispaa ya Kigoma Bw.Boniface Nyambele imetangazwa jana na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa George Simbachawene katika mkutano na waandishi wa habari baada ya tangazo kutolewa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ofisi ya Rais Tamisemi Rebecca Kwandu.
Kwa upande wake Mkrugenzi Mtendaji Manispaa ya Mpanda Bw.Suleiman Lukanga anayekabiliwa na tuhuma za ununuzi hewa wa gari la kusomba taka kwa Sh milioni 92.75 na ubadhirifu wa fedha za ujenzi wa skimu ya umwagiliaji ya Kakese, Sh milioni 294.
Naye Mkurugenzi Boniface Nyambele wa manispaa ya Kigoma anayekabiliwa na tuhuma za uuzaji wa nyumba za halmashauri bila kufuata sheria, kanuni na taratibu zilizopo, zinazomtaka awe na kibali cha waziri mwenye dhamana.   
Nafasi ya Mkurugenzi Mtendaji Manispaa ya Mpanda itakaimiwa na Lauteri Kanoni ambaye ni Katibu Tawala Msaidizi kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi huku nafasi ya Mkurugenzi Manispaa ya Kigoma ikikaimiwa na Sultan Ndilowa ambaye ni Mkuu wa Idara ya Maji Manispaa ya Kigoma
Aidha,Waziri Simbachawene amewataka wakurugenzi watendaji wa mamlaka za serikali za mitaa nchini kuwa makini katika kutekeleza majukumu yao kwa kufuata sheria, kanuni na taratibu zilizopo.
Amesema serikali haitasita kuchukua hatua za kinidhamu kwa watumishi wote,ambao watakiuka matakwa ya sheria, kanuni na taratibu na kutoweka mbele maslahi ya umma.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA