WACHIMBAJI DHAHABU ZAIDI YA 200 MPANDA WAPIGWA MARUFUKU UCHIMBAJI,VITENDO VYA WIZI VYAIBUKA


Na.Issack Gerald-Mpanda
Wachimbaji  wadogowadogo wa dhahabu katika mgodi wa Kampuni Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi wamesikitishwa na kitendo cha serikali kuwapiga marufuku uchimbaji wa madini katika mgodi huo kwa madai kuwa eneo hilo ni miliki ya makambi ya jeshi.

Hayo yamebainishwa na wachimbaji hao wakati wakizungumza na P5 TANZANIA MEDIA Sambamba na Mpanda Radio  mgodini hapo kuhusu namna wanavyoathirika kutokana na kufukuzwa katika mgodi huo.
Wamesema kuwa wanategemea mgodi huo kuendesha maisha ya kila siku ikiwemo kusomesha watoto na kulipia kodi ya nyumba.
Mwenyekiti wa mtaa wa Kampuni Bw.Simon James amesema kuwa,kufukuzwa kwa wachimbaji hao wapatao 200 kumepelekea vitendo vya wizi kuibuka ambapo jana mifugo ikiwemo nguruwe na mbuzi kadhaa wameibwa katika makazi ya watu.
Kwa mjibu wa maelezo ya wajimbaji hao walioanza kuchimba eneo hilo miaka ya 1980 wamesema kuwa wanategemea kuendesha maisha kutokana na mgodi huo.
Baadhi ya wachimbaji wadogo ambao wamezungumzia khusu wanavyoathiliwa na kufukuzwa katika mgodi huo ni pamoja na Athman Omary,Lucas Juma,Nuru Hassan na Faustin Method Kamatasimba
Kwa upande wake Mjumbe wa seriklai ya Mtaa wa Kampuni Bi.Flora Simon Mpenda,amesema kuwa kufukuzwa kwa wachimbaji hao kumeathiri mapato ya kuendesha shule ya Msingi Sambwe.
Kwa upande wake Meya wa Manispaa ya Mpanda Bw.Wilium Philipo Mbogo amesema kuwa suala hili lipo katika mamlaka husika kwa mazungumzo  ili lipatiwe ufumbuzi.
Wiki iliyopita,madiwani wa balaza la Manispaa ya Mpanda kupitia kikao chake cha januari 14 mwaka huu waliiomba Manispaa ya Mpanda kuweka mipaka kati ya eneo la  jeshi na makazi ya raia ili kuondoa migogoro ya ardhi.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA