JAMII NSIMBO YAOMBWA KUSHIRIKI MATENGENEZO YA MIUNDOMBINU YA BARABARA



Na.Vumilia Abel-Nsimbo
JAMII wilayani Nsimbo mkoani katavi imeombwa kushiriki katika matengenezo madogo madogo ya miundombinu ya barabara.

Ushauri huo umetolewa na  mkurugenzi wa halmashauri ya Nsimbo Bw Michael Nzyungu wakati akizungumza na  P5 TANZANIA sambamba na mpanda radio Ofisini kwake.
Amesema, hali  ya  miundombinu ya barabara hairidhishi  kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha  na kuwa baadhi hazikusajiliwa wala kutengewa bajeti, na zipo katika mikakati ya kusajiliwa ili zipatiwe bajeti kwa mwaka wa fedha 2016 /2017.
Bw. Nzyungu  amezitaja  baadhi ya barabara zilizotengewa bajeti ni Itenka, Magamba, Kasalala, Sungamila, Katumba complex1 na  Katumba complex B, Urwila na Usense.
Aidha, amewataka madiwani na watendaji  waonapo dalili hatarishi ya kuharibika miundombimu hiyo watoe taarifa mapema ili hatua zichukuliwe.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA