MKOA WA KATAVI KUTOA SEMINA KWA VIONGOZI WA NGAZI ZA MITAA ILI KUTAMBUA MAJUKUMU YAO


Na.Boniface Mpagape:Mpanda
SERIKALI Mkoani katavi inatarajia kutoa semina kwa viongozi wa serikali kuanzia ngazi za vijiji, kata na tarafa ili watambue vyema majukumu yao.

Mkuu wa mkoa wa katavi Dk. Ibrahim Msengi amesema hayo wakati akizungumza na P5 TANZANIA MEDIA Sambamba na Mpanda radio ofisini kwake. Amesema imebainika kuwa baadhi ya viongozi wa serikali katika ngazi hizo mkoani Katavi wamekuwa hawatambui vizuri majukumu na mipaka ya madaraka waliyonayo.
Amesema semina hiyo inayotarajiwa kufanyika hivi karibuni itawajengea uwezo wa kutambua uwajibikaji wao kwa wananchi na kurahisisha utendaji kazi.
Aidha Mkuu wa mkoa wa Katavi amesema semina hiyo itakuwa ni chachu ya kuleta mabadiliko katika ngazi za uongozi kwani wahusika watapaswa kutoa taarifa kuhusu utendaji wao na itakuwa rahisi kupima uwajibikaji wao katika shughuli za maendeleo.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA