MATUKIO 6 MAKUU YALIYOTOKEA KATAVI WIKI HILI LA SITA-JAMII YATAKIWA KUWATAMBUA WATOTO WENYE ULEMAVU

Na.Issack Gerald-MPANDA.
JAMII Mkoani Katavi imeombwa kutambua uwepo wa watoto wenye ulemavu, ili kuwapatia haki za msingi sawa na  watoto wengine.

Ombi hilo limetolewa na Mratibu Elimu jumuishi Mkoa wa Rukwa na katavi Raphael Fortunatus wakati akizungumza na P5 TANZANIA Alhamisi ya wiki hii katika ofisi za  Shirika la IFI lililopo Manispaa ya Mpanda Mkoani hapa.
Amesema shirika la hilo  linafanya kazi ya kubaini na kutambua uwepo wa watoto hao, kuwaandikisha shule na kutoa elimu kwa watoto hao na jamii kwa ujumla juu ya haki za watoto wenye  walemavu.

Aidha bw. Fortunatus amesema kupiatia mikutano ya hadhara, pamoja na Mabaraza ya watoto wenye ulemavu, Shirika la IFI limewafikia watoto 112 na kuwapatia misaada mbalimbali.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA