MATUKIO 6 MAKUU YALIYOTOKEA KATAVI WIKI HILI LA PILI-WANNE WASHIKILIWA NA POLISI KATAVI KWA KUPORA ZAIDI YA MILIONI 7,SILAHA ZA KIVITA PIA ZAKAMATWA

Na.Issack Gerald -KATAVI
Jeshi la Polisi Mkoani Katavi linawashikilia watu wanne wanaosadikika kuwa majambazi Wilayani Mpanda kwa tuhuma za kujeruhi na kupora kiasi cha shilingi milioni saba.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani Dhahiri Kidavashari,amesema Jumatatu ya wiki hii kuwa tukio hilo limetokea katika kijiji cha Vikonge kata ya Kabungu.
Kamanda Kidavashari aliwataja waliokamatwa katika msako wa jeshi la polisi kuwa ni Mayunga Saguda Makobo(44) mkazi wa Mnyagala,Halila Tiga Bujoribu(33) na Mnyaga Maziku(30) wakazi wa Luhafe na Shija Mahoma(30) mkazi wa Kawajense.
Amesema watu hao wanaosakika kuwa majambazi walikuwa wakitumia silaha mbili za kivita aina ya SMG UA-3379 yenye risasi 13 na SMG namba 19111685 yenye risasi 23 ambazo zote zimekamatwa.

Wakati huohuo wakazi Mkoani     Katavi wametakiwa kuendelea kutoa ushirikiano kwa jeshi la Polisi kubaini uharifu.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA