TUNDU LISSU KUFANYIWA UPASUAJI WA GOTI



Mbunge wa Singida Mashariki (CHADEMA),Tundu Lissu anatarajiwa kufanyiwa upasuaji mwingine wa goti la kulia Machi 14,2018 katika Hospitali ya Chuo kikuu cha Leuven, Gasthuisberg ili kumnusuru asipatikane na athari za mifupa kutojiunga kwa wakati.

Lissu amebainisha hayo usiku wa kuamkia leo wakati alivyokuwa anawafahamisha umma juu ya maendeleo ya afya yanavyoendelea huko alipo na kusema anaendelea vizuri na matibabu na sasa anaweza kusimama kwa miguu yote miwili bila ya msaada wa magongo ya kutembelea.
Mbunge Tundu Lissu alishambuliwa na watu wasiojulikana tangu Septemba 7,2017 akiwa mkoani Dodoma na kisha kupelekwa nchini Nairobi kwa matibabu na baada ya miezi 3 alipelekwa nchini Ubelgiji kwa hatua nyingine ya matibabu.
Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED 

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA