RAIS JOHN MAGUFULI ATOA AGIZO KWA WAZIRI WA VIWANDA,BIASHARA NA UWEKEZAJI



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Dkt.John Magufuli amemwagiza Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji,Charles Mwijage kuhakikisha wamiliki wa viwanda vya ndani wanaajiri wazawa.

Ametoa agizo hilo leo Jumapili Machi 11,2018 wakati akizindua kiwanda cha kufua vyuma cha Kahama Oil Mill mjini Kahama mkoani Shinyanga.
Rais amesema wananchi wazawa ndio waliompigia kura,hivyo wapewe kipaumbele cha ajira katika viwanda hivyo huku akiwataka wamiliki wa viwanda kuhakikisha wanatumia malighafi za ndani kutengeneza bidhaa badala ya kuagiza kutoka nje ya nchi.
Kuhusu kiwanda cha chuma amesema malighafi inapatikana nchini,hivyo iwapo mkurugenzi wa Kahama Oil Mill anahitaji yupo tayari kumpa bure badala ya kuagiza nje.
Wakati huo huo amewataka Watanzania kununua bidhaa za ndani ambapo amewataka wamiliki wa viwanda kutengeneza zenye ubora ili kuhimili ushindani.
Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED 

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA