RAIS MAGUFULI ASEMA ANAPATA TABU


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dk. John Pombe Magufuli amekiri kupata wakati mgumu katika uteuzi wa Baraza la Mawaziri kutokana na kuwa Mkoa wa Singida kujaa Wabunge wenye sifa zote za kushika nyadhifa hizo.
Akiwa katika uzinduzi wa kiwanda cha mafuta ya alizeti mkoani  Singida,Rais Magufuli amesema kwamba anafurahishwa sana na utendaji kazi wa wabunge hao kiasi kwamba alitamani kuwateua wote kuwa katika baraza lake.
Rais amesema kwamba Wabunge wa mkoa huo wamekuwa wakimfurahisha katika utendaji kazi wao wa kuwatumikia wananchi.
Aidha Rais Magufuli amekiri kufurahishwa na wakazi wa Singida kwani wamekuwa wakitekeleza kauli ya 'Hapa Kazi Tu' kwa vitendo kwa  kulima sehemu kubwa ya mkoa huo ambapo amejionea mwenyewe akiwa katika safari ya gari kuelekea mkoani hapo.
Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA