BARAZA LA MADIWANI LACHARUKA UPIGAJI CHAPA MIFUGO CHINI YA KIWANGO


BARAZA la madiwani wa halmashauri ya Wilaya ya Iramba mkoani Singida limewajia juu wataalamu wake kwa kutotekeleza kwa weledi upigaji chapa mifugo na kuwatishia kuwa watalamika kwenda kurudia zoezi hilo kwa gharama zao iwapo alama zinazowekwa zitafutika baada ya muda mfupi. 
Katika kikao cha baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba kilichofanyika Mjini Kiomboi, ajenda iliyochukua uzito mkubwa ni juu ya kufutika kwa alama zilizowekwa kwenye upigaji chapa mifugo na kuchelewa kwa malipo ya wananchi walioshiriki  kusaidia  utekelezaji wa zoezi hilo. 
Afisa mifugo Wilaya ya Iramba Andrew Manyerere anasema kuwa ingawa zoezi hilo lilitekelezwa kwa kuzingatia sheria lakini kwa mifugo ambayo alama zake zimefutika watarudia  bila malipo.
Hata hivyo uamuzi wa baraza la madiwani wa uliotolewa na Mwenyekiti wake Simion Tyosela ni kwa wataalamu kufanyakazi hiyo kwa weledi vinginevyo watarudia zoezi hilo kwa gharama zao.
Zaidi ya shilingi milioni 16 zimetumika kuwalipa wanachi waliosaidia zoezi hilo ambapo jumla ya ng’ombe 190,000 wamepigwa chapa katika kipindi cha kuanzia Julai mwaka jana hadi Januari mwaka huu.
 Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED


Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA