SERIKALI MKOANI KIGOMA IMETATUA TATIZO LA UHABA WA ARDHI

Jumla ya Hekta Elfu 10  sawa na hekari 26200 zimepunguzwa kutoka katika hifadhi ya Makere kusini wilayani Kasulu na Kugawiwa kwa wananchi wa vijiji  vya Mvinza na Kagerankanda.
Hatua hiyo ni utekelezaji wa agizo la raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Magafuli alilolitoa mwezi july mwaka jana wakati wa ziara yake Mkoani Kigoma lengo likiwa ni kwaongezea wananchi ardhi kwa ajili ya shughuli zakilimo.
Akimwakilisha Rais,kaimu mkuu wa wilaya ya Buhigwe mkoani Kigoma Kanal Malko Gaguti amesema,mara baada ya kufanya tathimini katika hifadhi hiyo imeonekana zaidi ya hekta 72 elfu za msitu wa Makere kusini kati ya hizo hekta elfu 18 zimeharibiwa vibaya kutokana na uvamizi wa shughuli za kilimo.
Wahamiaji wanoingia nchini kinyume na sheria imeonekana kuwa chanzo kikubwa cha uharibifu wa misitu lakini pia kufanywa kwa vitendo vya uharifu ambapo Gaguti ambapoa ametoa rai kwa wakazi wa vijiji Mvinza na Kagerankanda kutumia vizuri ardhi hiyo
Wakitoa shukrani kwa serikali kwa niaba ya wananchi kutokana na hatua iliyochukuliwa ya serikali kutoa eneo hilo kwa wananchi,diwani wa kata ya Kagerankanda Ezeki Mshingo na Mwenyekiti wa kijiji cha Mvinza Kalos Bukakiye wamesema serikali imetatua kilio cha wananchi cha muda mrefu ambapo wameahidi kutunza mipaka ya hifadhi hiyo.
Mwandishi:Isaac Aron Isaac
Mhariri:Issack Gerald

Habari zaidi ni kupitia P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA