JAMII WILAYANI MPANDA IMETAKIWA KUWAJALI WATU WENYE MAHITAJI MAALUMU

Na.Issack Gerald
Jamii mkoani katavi imetakiwa kuwajali watu wenye mahitaji maalumu ili kuwawezesha kushiriki katika shughuli mbalimbali za uzalishaji mali
Wito huo umetolewa na Afisa ustawi wa jamii wa Manispaa ya Mpanda Bi.Agness Bulaganya ambapo amesema idara ya ustawi wa jamii inaendelea kutoa elimu shirikishi ili kuhakikisha jamii inapata uelewa wa kuishi na watu walio katika makundi hayo.
Katika hatua nyingine Bi.Buraganya amesma endapo jamii inakuwa na mwamko wa kuwatambua watu walio kwenye makundi hayo,serikali mkoani Katavi iko tayari kuyaunganisha na fursa mbalimbali zitakazowawezesha kuijtegemea
Amesema kwa mwaka wa 2018 idara ya ustawi wa jamii mkoani Katavi imejipanga kushughulikia masuala mbalimbali ikiwemo kupunguza ongezeko la mimba za utotoni.
Kauli ya serikali kuhusu watu wenye mahitaji maalumu inakuja ikiwa ni siku moja baada ya shirikisho la vyama vya watu wenye ulemavu mkoani Katavi kusema kuwa serikali ya awamu ya tano haiwajali katika mahitaji yao kama inavyostahili hasa katika kusikiliza kero zao ikiwemo kuadhimisha siku maalumu zinazohusu makundi hayo ili wapate nafasi ya kueleza kero zao.

Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA