WASIOJULIKANA WAMEUA MTU KWA RISASI MKOANI KATAVI



Na.Issack Gerald-Tanganyika Katavi
ACP Damas Nyanda
Mtu mmoja anayefahamika kwa jila la Suzani Chales (40) mkaazi wa Kata ya Katuma wilaya ya Tanganyika Mkoani Katavi amekufa kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana.

Akithinitisha tukio hilo Kamanda wa Polisi Damasi Nyanda amesema tukio hilo limetokea jana usiku wa saa mbili wakati wanafamilia hao wakiangalia taarifa ya habari ambapo inadaiwa watu hao waliomba maji ya kunywa na baadaye kufanya uhalifu huo.

Mwanamke huyo ni mke wa mwenyekiti wa Chama  cha Wafugaji Mkoa wa  Katavi (CCWT).
Tukio lingine limetokea majira a sasa saba usiku katika kijiji cha Kabage B kilichopo wilayani Tanganyika Mama mmoja ameuwawa kwa kukatwa na Mapanga na watu wasio julikana.
Kamanda Nyanda amewaasa wananchi kutoa taarifa kwa jeshi la polisi pindi wanapo baini uwepo wa vitendo vya uharifu ili sheria ichukue mkondo wake.
Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Tanganyika Salehe Muhando amewataka wananchi wanao miliki silaha kinyume na utaratibu wazisalimishe katika jeshi la polisi kabla ya hatua kuchukuliwa.
Kumeendelea kujitokeza wimbi la uhalifu wa matumizi ya silaha za moto pamoja na matukio ya ukataji wa mapanga huku mengine yakihusishwa na imani za kishirikina Wilayani humo.
Habari zaidi ni www.p5tanzania.blogspot.com au ukurasa P5Tanzania Limited

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA