ULINZI SHIRIKISHI UMESAIDIA KUTOKOMEZA UHARIFU MKOANI TABORA



Emeelezwa kuwa kuwepo kwa vikundi vya ulinzi shirikishi katika wilaya mbalimbali za mkoa wa Tabora kumesaidia kupunguza vitendo vya uharifu vilivyokuwa vikifanywa na baadhi ya watu wasio waadilifu mkoani humo.

Hayo yamesemwa leo na kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Tabora kamishna msaidizi mwandamizi wa polisi ACP Wilbroad Mutafungwa.
Kamnada Mutafungwa amesema jeshi la polisi mkoani humo limekuwa likitoa askari mmoja kwa kila mtaa ambao unakikundi cha ulinzi shirikishi ili kuimarisha doria katika mitaa hiyo.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa jeshi la Sungu sungu katika kijiji cha Mwanihalanga kata ya Mbutu wilayani Igunga amesema katika kijiji chao hupanga watu kumi kwa ajili kushiriki kwenye ulinzi shirikishi wakati wa usiku na asiyetaka hutozwa faini.
Nao Baadhi ya wenyeviti na wajumbe wa serikali za mitaa mbalimbali mkoani humo wamesema wao hushirikiana vizuri na askari wa jeshi la polisi katika kuimalisha doria katika mitaa yao na kuwaripoti watu wageni wasiowatambua ambao hufika katika maeneo yao.
Mmoja wa wakazi waliowahi kuibiwa Bi Asha Jacobo kutokana na kutokuwepo kwa ulinzi shirikishi katika mtaa wake amesema ulinzi shirikishi katika jamii ni muhimu kwa kuwa bila ulinzi ndiyo maana hata yeye alibiwa mali yake.
Habari zaidi ni www.p5tanzania.blogspot.com au ukurasa P5Tanzania Limited

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA