WALIOUAWA KWA BOMU SOMALIA IMEFIKIA 358

Mlipuko wa bomu Somalia uliowauawa zaidi ya watu 350
Serikali ya Somalia imesema idadi ya watu waliokufa katika shambulio kubwa la bomu la ndani ya Lori katika mji mkuu Mogadishu Jumamosi iliyopita imeongezeka na kufikia hadi watu 358.
Lori lililipuka katika barabara ya makutano yenye shughuli nyingi na kuharibu hoteli,ofisi za serikali na migahawa .
Hata hivyo haijabainika ikiwa eneo hilo la makutano ndilo lililolengwa au dereva wa Lori alilipua vilipuzi kwa sababu tayari watu walikuwa wameanza kushuku lori lake .
Maafisa wamelilaumu kundi la wanamgambo wa al-Shabaab kwa shambulio hilo,lakini kundi hilo bado halijasema kuwa lilihusika na mlipuko huo

Mlipuko huo uliwajeruhi watu zaidi ya mia mbili

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA