MBUNGE JIMBO LA NSIMBO ATUHUMIWA KUJIHUSISHA NA RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA UVCCM WILAYANI MPANDA KATAVI -Septemba 27,2017

Mbunge Jimbo la Nsimbo Richard Mbogo
MBUNGE wa jimbo la Nsimbo wa jimbo la Nsimbo Richard Philipo Mbogo ametuhumiwa kuwa miongoni mwa watu waliohusika katika kutoa rushwa ya fedha kwa kila mjumbe aliyeshiriki katika uchaguzi wa viongozi wa Jumuiya ya Vijana ya chama cha Mapinduzi CCM Wilayani Mpanda.

Malalamiko hayo yametolewa leo na aliyekuwa Mgombea kwa nafasi ya mwenyekiti wa vijana Bw.Saimoni John Saimoni katika uchaguzi uliofanyika jana ambapo amekiri kuwepo kwa vitendo vya rushwa miongoni mwa viongozi na kusema hali hiyo ndiyo iliyomkwamisha kushinda kiti hicho.
Bw.Simon John Simon amemtuhumu mbunge wa jimbo la Nsimbo Richard Philipo Mbogo kuwa ni miongoni mwa waliokuwa wakihusika kutoa rushwa kwa wajumbe wa mkutano hadi shilingi elfu ishirini(20,000) kwa kila mjumbe aliyekuwa na sifa ya kupiga kura.
Hata hivyo mbunge wa jimbo la Nsimbo Richard Philipo Mbogo  amekanusha madai hayo na kusema kuwa kama kuna mtu au mgombea mwenye ushahidi wa vitendo hivyo vya Rushwa aende mahakamani ili kutoa ushahidi huo.
Kwa upande wa Msimamizi wa uchaguzi huo ambaye ni Diwani Kata ya Makanyagio Hidary Sumry amesema uchaguzi huo ulikuwa huru na haki na amewataka wenye malalamiko kuyapeleka katika vyombo husika.
Uchauzi

Habari zaidi ni www.p5tanzania.blogspot.com au Ukurasa P5Tanzania Limited

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA