CHADEMA WAENDELEA NA UCHAGUZI WA VIONGOZI NGAZI YA MITAA-Septemba 27,2017

Na.Issack Gerald-Mpanda Katavi
Chama cha demokrasia na maendeleo (Chadema) mkoani Katavi kimewataka wanachama wake kuwa watulivu katika kipindi cha uchaguzi mdogo unaojulikana kama chadema msingi.

Hayo yamesemwa na katibu wa chama hicho ngazi ya wilaya  Bw.Iddi Omary Faraji baada ya kutolea ufafanuzi wa sintofahamu kuhusu chaguzi mbalimbali ambazo zimekuwa zikiendelea katika vyama tofauti.
Aidha katibu ameelezea lengo la uchaguzi huo kuwa ni kutaka kujua wanachama walioingia pamoja na waliotoka ndani ya chama hicho.
Hata hivyo amewaomba wanachama kuonyesha ushirikiano ili kukijenga chama hicho.
Kwa mjibu wa kiongozi huyo,chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema kinatarajia kufanya chaguzi mbalimbali katika ngazi ya mitaa mpaka watakapofanya uchaguzi wa kupata viongozi wa kitaifa ifikapo mwezi Oktoba mwaka 2017

Habari zaidi ni www.p5tanzania.blogspot.com au Ukurasa P5Tanzania Limited

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA