WAKAZI KIJIJI CHA MILALA MANISPAA YA MPANDA WALIA NA TATIZO LA UKOSEFU WA MAJI SAFI NA SALAMA-Julai 18,2017

Wakazi wa kijiji cha milala kilichopo Kata ya Misunkumilo Manispaa ya Mpanda wanashindwa kufanya shughuli za maendeleo kutokana na kutumia muda mwingi kutafuta maji.

Baadhi ya wakazi hao wakiwemo Deusi Abel na Justina Petro wamesema kuwa tatizo la ukosefu wa maji safi na salama ni la muda mrefu na kwamba mamlaka zimeishia kutoa ahadi bila utekelezaji.
Kwa upande wake diwani wa kata hiyo Mh.Matondo Alfred amekili kuwepo kwa tatizo hilo ambapo amefafanua kuwa kuwa eneo hilo limepewa kipaumbele katika bajeti ya utekelezaji wa shughuli za kimaendeleo ndani ya kata yake.
Sera yamaji katika jamuhuri ya muungano wa Tanzania inaelekeza kupatikana kwa maji kila umbali wa mita mianne jambo ambalo mpaka sasa halijatekelezwa.


Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA