WAKAZI HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA WATAKIWA KUWA WAVUMILIVU SUALA LA BOMOABOMOA KUPISHA RELI-Julai 18,2017

Manispaa ya Tabora
Wakazi wa halmashauri ya manispaa ya Tabora ambao nyumba zao zimewekewa alama kwa ajili ya kubomolewa wametakiwa kuwa wavumilivu wakati kamati iliyoundwa kufuatilia zoezi la kubomoa ili kupisha ujenzi wa reli ya kisasa kukamilisha kazi yake.

Rai hiyo imetolewa na mbunge wa Tabora mjini Mh Emanuel Mwakasaka katika mkutano wa hadhara na wananchi wa kata ya Tambuka reli kwa kumchagua kuwaongoza wananchi katika awamu ya tano
Mh.Mwakasaka amesema kamati iliyoundwa na mkuu wa Mkoa wa Tabora Bw.Agrey Mwanri ambaye ndiye mwenyekiti wake inaandaa mapendekezo kuhusiana na kubomolewa kwa nyumba zilizojengwa kando kando ya reli pia katika maeneo yote ya Shirika la reli Tanzania TRL
Mh Mwakasaka ambaye pia ni mwanasheria katika taaluma,amesema kwa mujibu wa sheria za nchi wananchi ambao wamejenga na kuishi kwenye maeneo hayo zaidi ya miaka kumi na mbili wanapaswa kufikiriwa na serikali ili walipwe fidia
Bonyeza P5TANZANIA.BLOGSPOT.COM uhabarike zaidi

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA