HOSPITALI YA MANISPAA YA MPANDA LAWAMANI KWA UNYANYASAJI DHIDI YA WAGONJWA WANAOHITAJI KUONGEZEWA DAMU-Julai 18,2017

Baadhi ya wananchi halmashauri ya manispaa ya Mpanda mkoani Katavi,wamelalamikia hosipitali ya wilaya ya Mpanda kutokana na kuwepo kwa vikwazo vingi kwa  wagonjwa wenye upungufu wa damu.

Wakizungumza na Mpanda Radio,baadhi ya ndugu wanaouguza wagonjwa wao,wamesema mara baada ya wagonjwa wao kuongezewa damu hulazimiwa hulazimishwa kurudisha chupa nne za damu ili kufidia damu iliyotumika.

Katika hatua nyingine wananchi hao ambao hawakutaka majina yatajwe wamesema,gharama za matibabu zimepanda badala ya kushuka kama wizara ya afya hapa nchini inavyoagiza ambapo wamesejma baadhi hujinunulia vifaa tiba,mipira na chupa za kuhifadhia damu.

Kwa upande wake mganga mkuu wa hospitali ya Manispaa ya Mpanda Dk.Theopister Elisa amesema,lengo kuu la kuweka utaratibu huo hospitalini hapo ni kupata akiba ya damu salama ili kuwasaidia wangonjwa wenye uhitaji wa haraka wa kuongezewa damu wanaopelekwa hospitalini hapo. 

Habarika zaidi kupitia P5TANZANIA.BLOGSPOT.COM

Mawasiliano:p5tanzania@gmail.com

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA