LEO NI SIKU YA MTOTO WA KIKE DUNIANI MAADHIMISHO KITAIF AKUFANYIKA SHINYANGA,MIKOA 21 INAONGOZA KWA MIMBA ZA UTOTONI KINARA NI SHINYANGA KWA ASILIMIA 59.



Na.Issack Gerald Bathromeo Mashama
LEO ni siku ya mtoto wa kike duniani ambapo siku hiyo kitaifa inaadhimishwa Mkoani Shinyanga.

Katika maadhimisho hayo yanayolenga kuangazia matatizo yanayomkumba mtoto wa kike,Katibu mkuu wa Wizara ya afya,maendeleo ya jamii,jinsia wazee na watoto Sihaba Nkinga akiwa Wilayani Kahama,ameitaka jamii kutambua haki za mtoto wa kike na kuwataka kutowaozesha wakiwa chini ya umri mdogo.
‘’Bado changamoto moja inayokuta mtoto wa kike ni ndoa na mimba za utoto ambayo kama taifa hatuwezi kukubaliana nayo hatua nyingi tumefanaya lakini changamoto hii bado hatujaweza kuiondoa kabisa,tumeweza kupunguza kwa kiasi lakini pia takwimu nyingine zimeendelea kutuonesha kuwa  miaka ijayo kutakuwa na watoto wengi zaidi ambao watakatishwa ndotpo zao’’
Mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa kike anatarajiwa kuwa Mh.Ummy Mwalimu na kauli mbiyu mwaka huu ni “Mimba na Ndoa za Utotoni Zinaepukika: Chukua Hatua Kumlinda Mtoto wa Kike’’
Takwimu zinaonesha mkoa wa Shinyanga unaongoza kwa ndoa za utotoni, ukiwa na asilimia 59 ukifuatiwa na Tabora (58), Mara (55), Dodoma (51), Lindi (48), Mbeya (45), Morogoro (42), Singida (52), Rukwa (40), Ruvuma (39), Mwanza (37).
Mikoa mingine inayoongoza ni pmaoja na, Kagera (36), Mtwara (35), Manyara (34), Pwani (33), Tanga (29), Arusha (27), Kilimanjaro (27), Kigoma (29), Dar es Salaam (19) na Iringa (8).
Siku ya mtoto wa kike ilianzishwa rasmi na umoja wa mataifa mwaka 2012
Endelea kuwa name kufahamu kitakachojili kupitia P5TANZANIA.BLOGSPOT.COM
Kwa maoni au ushauri tuma kupitia p5tanzania@gmail.com

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA