KUHUSU KATAVI NA SIKU YA MTOTO WA KIKE DUNIANI LEO OKTOBA 11,2016-P5 TANZANIA INAKUSOGEZEA



Na.Issack Gerald Bathromeo Mashama-Katavi
ZAIDI ya makosa 100 ya unyanyasaji kwa mtoto wa kike yameripotiwa katika kipindi cha miezi 9 iliyopita ikiwa ni pamoja na makosa ya ubakaji,kutupa watoto,kuwapa mimba wanafunzi na kuwaachisha masomo.

Takwimu hizi ni kwa mjibu wa Mkuu wa dawati la jinsia na watoto Mkoani Katavi Afande Thobias Lindege ambazo amezitoa leo.
Kwa mjibu wa takwimu za umoja wa Matifa tangu kuanzishwa kwa siku ya mtoto wa kike duniani mwaka 2012,Tanzania inashika nafasi ya 3 kati ya nchi wanachama wa umoja wa mataifa 193 ikiongoza kwa kuwa mimba za utotoni ambapo mara nyingine huambatana na vifo kutokana na maumbile changa ya watoto walio chini ya umri wa miaka 18.
Maadhimisho ya siku ya mtoto wa kike duniani hufanyika kila mwaka Oktoba 11 ambapo kwa Tanzania maadhimisho haya yamefanyika Mkoani Shinyanga mkoa unaoongoza kwa mi,mba za utotoni kwa asilimia 59 ukifuatiwa na Tabora wenye asilimia 58.
Kauli mbiyu mwaka huu ni “Mimba na Ndoa za Utotoni Zinaepukika: Chukua Hatua Kumlinda Mtoto wa Kike’’
Endelea kuhabarika P5TANZANIA.BLOGSPOT.COM
Kwa maoni au ushauri tuma kupitia p5tanzania@gmail.com

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA