RIPOTI YA PILI BWENI LA WAVULANA SHULE YA SEKONDARI SANNY YA KANISA LA (KKKT) ILIYOPO MKOANI KATAVI KUTEKETEA KWA MOTO HII HAPA,TATHMINI YA AWALI MALI ZA SHILINGI MILIONI 8.97 ZILITKETEA


Na.Issack Gerald-Mpanda
Shule ya sekondari ya Sanny inayomilikiwa na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) imesema kuwa thamani ya awali ya mali za wanafunzi zilizoteketea kwa moto katika bweni la wavulana ni Milioni nane laki tisa na sabini elfu.
                                                  
Mwonekano wa Sehemu ya bweni la wavulana lililoteketea kwa moto Shule ya Sekondari Sanny Tarehe 11.02.2016

Tathmini hiyo imetolewa leo na Mkuu wa Shule hiyo Sister Anna Usiri wakati akizungumza na P5 TANZANIA MEDIA Ofisi kwake.
Sister Usiri ametaja baadhi ya mali zilizoteketea kwa moto katika tukio lililo Februari 11 mwaka huu kuwa ni pamoja na magodoro,vitanda na sare za wanafunzi.
Wakati huo huo amesema kuwa tathmini ya tukio hilo itatolewa hivi karibuni baada ya mahandisi kufanya uchunguzi na jingo lote lililoteketea.
Halikadhalika mkuu wa huyo wa shule amesema kuwa huenda tatizo hilo lilitokana na  kutokea kwa tetemeko lililosababisha nyaya za umeme kugusana na kusababsha moto huo.
Hata hivyo Jeshi la polisi Mkoani Katavi limesema kuwa bado linaendelea na uchunguzi ili kubaini chanzo cha moto ulioteketeza bweni hilo lililokuwa na wanafunzi 31.
Hata hivyo mpaka sasa,hajapata msaada wowote kutoka kwa wadau zaidi ya Mkuu wa Mkoa kuahidi magodoro saba kwa wanafunzi walio athilika  lakini hajaona chochote.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA